Nafasi za Kazi 13 Halmashauri ya Wilaya ya Geita November 2025

Job Role Insights

  • Date posted

    2025-11-06

  • Closing date

    2025-11-18

  • Hiring location

    Geita

  • Career level

    Middle

  • Qualification

    Bachelor Degree Certificate Degree Diploma

  • Experience

    1 - 2 Years

  • Quantity

    10 person

  • Gender

    both

  • Job ID

    124703

Job Description

OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

Kumb. Na. HB.9/150/01/02 05/11/2025

TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri (W) ya Geita anawatangazia Watanzania wenye sifa kuomba nafasi za kazi kumi na tatu (13) katika Halmashauri hii baada ya kupata kibali kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa mchanganuo ufuatao:

The Executive Director of the Geita District Council is inviting applications from qualified Tanzanian citizens for a total of thirteen (13) vacant posts. The positions available are Records Assistant Grade II (4 openings) and Driver Grade II (9 openings). Applications must be submitted through the electronic recruitment portal by the deadline of November 18, 2025.


1.0 MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA II - NAFASI 4

1.1 MAJUKUMU YA KAZI

  • Kutafuta kumbukumbu/nyaraka/mafaili yanayohitajika na wasomaji.
  • Kudhibiti upokeaji, uandikishaji wa Kumbukumbu/nyaraka.
  • Kuchambua, kuorodhesha na kupanga kumbukumbu/nyaraka katika makundi kulingana na somo husika (Classification and Boxing) kwa ajili ya matumizi ya ofisi.
  • Kuweka/kupanga kumbukumbu/nyaraka katika reki (File Racks/Cabinets) katika masjala/vyumba vya kuhifadhia kumbukumbu.
  • Kuweka kumbukumbu (barua, nyaraka nk) katika mafaili.
  • Kushughulikia maombi ya Kumbukumbu/Nyaraka kutoka Taasisi za Serikali.
  • Kutekeleza kazi zozote atakazokuwa amepangiwa na Msimamizi wake wa kazi.

1.1.2 SIFA ZA MWOMBAJI Awe amehitimu Elimu ya Kidato cha Nne (Form IV) au cha Sita (Form VI), awe na mafunzo ya Stashahada ya Utunzaji wa Kumbukumbu katika fani ya Masjala kutoka vyuo vinavyotambuliwa na Serikali.

1.1.3 NGAZI YA MSHAHARA

TGS C.


2.0 DEREVA DARAJA LA II - NAFASI 9

2.1 MAJUKUMU YA KAZI

  • Kukagua gari kabla na baada ya safari ili kubaini hali ya usalama wa gari.
  • Kuwapeleka watumishi maeneo mbalimbali kwenye safari za kikazi.
  • Kufanya matengenezo madogomadogo ya gari.
  • Kukusanya na kusambaza nyaraka mbalimbali.
  • Kujaza na kutunza taarifa za safari zote katika daftari la safari.
  • Kufanya usafi wa gari.
  • Kufanya kazi nyingine kadri atakavyoelekeza na Msimamizi wake.

2.1.2 SIFA ZA MWOMBAJI Kuajiriwa wenye cheti cha Kidato cha Nne (Form IV) na Leseni ya Daraja E au C ya uendeshaji magari ambayo wamefanyia kazi kwa muda usiopungua mwaka mmoja (1) bila kusababisha ajali pamoja na vyeti vya mafunzo vilivyowapatia sifa ya kupata madaraja husika. Wawe wamehudhuria mafunzo ya msingi ya Uendeshaji magari (Basic Driving Course) yanayotolewa na Chuo cha VETA au Chuo kingine kinachotambuliwa na Serikali.

2.1.3 NGAZI YA MSHAHARA

TGS B.


MASHARTI YA JUMLA

  • Waombaji wote wawe raia wa Tanzania na wenye umri kuanzia miaka 18 na usiozidi miaka 45 isipokuwa kwa wale tu walioko kazini Serikalini.
  • Waombaji wenye ulemavu wanahamasishwa kutuma maombi na wanapaswa kuainisha kwenye Mfumo wa kuombea ajira ulemavu walionao kwa ajili ya taarifa kwa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma.
  • Waombaji wote waambatishe maelezo binafsi yaliyojitosheleza (Detail Curriculum Vitae) yenye anuani inayotumika, namba za simu zinazopatikana na Anuani ya Barua pepe (E-mail address) pamoja na majina ya wadhamini (Referees) watatu wa kuaminika.
  • Maombi yote yaambatane na vyeti vya Elimu na Taaluma vilivyothibitishwa na Mwanasheria/Wakili ambavyo ni vyeti vya Kidato cha Nne au Sita kwa wale waliofikia kiwango hicho na vyeti vya kuhitimu mafunzo mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika:
    • Postgraduate/Degree/Advanced Diploma/Diploma/Certificates
    • Cheti cha Mtihani wa Kidato cha IV na VI
    • Computer Certificate
    • Vyeti vya Kitaaluma (Proffessional Certificate from Respective Boards)
  • Testimonials, Provisional Results, Statements of Results, Hati za Matokeo ya Kidato cha Nne na Kidato cha Sita (FORM IV and FORM VI RESULTS SLIPS) HAZITAPOKELEWA.
  • Waombaji waliosoma nje ya Nchi wahakikishe vyeti vyao vinahakikiwa na vimethibitishwa na Mamlaka husika (TCU, NECTA na NACTE).
  • Waombaji waliostaafishwa katika Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba isipokuwa kama wana Kibali kutoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi.
  • Waombaji kazi ambao tayari ni waajiriwa katika nafasi za kuingilia walioko katika Utumishi wa Umma wasiombe na wanatakiwa kuzingatia maelekezo yaliyo katika Waraka Na. CAC.45/257/01/D/140 wa tarehe 30 Novemba, 2010.
  • Uwasilishaji wa taarifa na sifa za kughushi wahusika watachukuliwa hatua za kisheria.
  • Wasailiwa ambao majina yao yanatofautiana katika nyaraka zao wanapaswa kuwasilisha Hati ya Kiapo cha Kubadili Jina (Deed Poll) iliyosajiliwa na Wizara ya Ardhi.
  • Mwisho wa kutuma maombi ni tarehe 18 Novemba, 2025.
  • Maombi yote yatumwe kwenye mfumo wa kielektroniki wa Ajira (Recruitment Portal) kupitia anuani ifuatayo: https://portal.ajira.go.tz/. Anuani hii inapatikana pia kwenye tovuti ya Sekretarieti ya Ajira kwa kuingia sehemu iliyoandikwa "Recruitment Portal".
  • Maombi yatakayowasilishwa nje ya utaratibu ulioainishwa katika tangazo hili HAYATAFANYIWA KAZI.

MUHIMU: Kumbuka kuambatisha barua yako ya maombi ya kazi iliyosainiwa pamoja na vyeti vya elimu, anuani ya barua hiyo ielekezwe kwa: -

Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Geita, S.L.P 139, Geita

Interested in this job?

12 days left to apply

Apply now

Share this opportunity

Help others find their dream job

How to Apply

Apply now
Whatsapp-color Created with Sketch. Job Alert
Subscribe to receive instant alerts of new relevant jobs directly to your WhatsApp.
Subcrible
Send message
Cancel