Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi anapenda kuwataarifu waombaji kazi wote walioomba kazi kuwa usaili unatarajiwa kuendeshwa kuanzia tarehe 23/06/2026 hadi 24/06/2026, na hatimaye kuwapangia vituo vya kazi waombaji watakaofaulu usaili huo.
Wasailiwa wanaoitwa kwenye usaili wanapaswa kuzingatia maelekezo yafuatayo:
- Usaili utafanyika kuanzia tarehe kama ilivyooneshwa kwenye tangazo hili. Muda na sehemu ambapo usaili utafanyika umeainishwa kwa kila kada.
- Kila msailiwa anatakiwa kufika kwenye eneo la usaili akiwa amevaa barakoa (mask).
- Kila msailiwa anapaswa kuwa na kitambulisho kwa ajili ya utambuzi.
Vitambulisho vinavyokubalika ni pamoja na:
- Kitambulisho cha Mkazi
- Kitambulisho cha Mpiga Kura
- Kitambulisho cha Kazi
- Kitambulisho cha Uraia
- Hati ya Kusafiria
- Leseni ya Udereva
- Barua ya Utambulisho kutoka Serikali ya Mtaa/Kijiji anachotoka
- Wasailiwa wanatakiwa kufika na vyeti vyao halisi, kuanzia:
- Cheti cha Kuzaliwa
- Cheti cha Kidato cha IV
- Cheti cha Kidato cha VI
- Astashahada
- Stashahada
- Stashahada ya Juu
- Shahada na kuendelea kutegemeana na sifa za nafasi husika
- Wasailiwa watakaowasilisha:
- Testimonials
- Provisional Results
- Statement of Results
- Form IV Results Slip
- Form VI Results Slip
Havitakubaliwa na hawataruhusiwa kuendelea na usaili.
- Kwa kada zinazohitaji usajili wa Bodi za Kitaaluma, wasailiwa wanapaswa kuja na:
- Vyeti vyao halisi vya usajili
- Leseni za kufanyia kazi
- Kila msailiwa atajigharamia:
- Chakula
- Usafiri
- Malazi
Aidha, kila msailiwa anapaswa kuhudhuria usaili akiwa na mavazi nadhifu na yenye staha kulingana na waraka wa mavazi.
- Wasailiwa waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe vyeti vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa na mamlaka husika kama:
- TCU
- NACTVET
- NECTA
Wasailiwa wa kada zinazohitaji GPA waliosoma nje ya Tanzania wawasilishe cheti cha ukokotozi wa GPA kutoka TCU.
- Wasailiwa ambao hawajaona majina yao kwenye tangazo hili wanapaswa kuingia kwenye akaunti zao za Ajira Portal na kuona sababu za kutokuitwa kwao ili wasikose fursa wakati mwingine.
- Wasailiwa wote walioitwa kwenye usaili wahakikishe wanaingia kwenye akaunti zao na kunakili namba ya usaili.
Aidha, wasailiwa watakaofanya usaili wa mchujo kwa njia ya mtandao wanapaswa kukumbuka:
- Barua pepe (email address) zao
- Nywila (password) zao
wanazotumia katika mfumo wa Ajira Portal.
- Wasailiwa ambao majina yao yanatofautiana katika nyaraka zao wanapaswa kuwasilisha Hati ya Kiapo cha Kubadili Jina (Deed Poll) iliyosajiliwa na Wizara ya Ardhi.
- Waombaji wote wa kazi wanakumbushwa kuwa ni marufuku:
- Kutoa rushwa
- Kupokea rushwa kwa lengo la kupata ajira au kupangiwa kituo cha kazi.
Mchakato wa ajira unazingatia misingi ya:
- Haki
- Usawa
- Uwazi
kwa kuzingatia sifa stahiki zilizoainishwa katika tangazo la kazi husika na muundo wa utumishi wa idara inayohusika.
