Overview
Jawabu Financial Services Limited ilisajiliwa mnamo tarehe 16/03/2022 na msajili wa makampuni na kupata namba ya usajili 155509155.
Jawabu Financial Services Limited inajishughulisha na utoaji wa mikopo kwa wajasiriamali wadogo Tanzania Bara kwa lengo la kuwawezesha kukuza mitaji na kuendeleza biashara zao. Imepata kibali namba MSP2-A39 kutoka Benki Kuu ya Tanzania kwa ajili ya kuendesha biashara ya kutoa mikopo midogo kwa kuzingatia Sheria ya Huduma Ndogo za Fedha (Microfinance Act, Cap. 407) ya mwaka 2018, na Kanuni za Huduma Ndogo za Fedha (Microfinance Regulations) za mwaka 2019.
