Tangazo la Kuitwa Kazini Taasisi Mbalimbali za Umma 19-12-2025
Job Role Insights
-
Date posted
2025-12-20
-
Closing date
2026-01-02
-
Hiring location
Tanzania
-
Quantity
1 person
-
Gender
both
-
Job ID
126369
Job Description
Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma anapenda kuwataarifu waombaji kazi wa nafasi mbalimbali waliofanya usaili kati ya tarehe 09-11-2024 na tarehe 17-10-2025 kuwa matokeo ya waombaji kazi waliofaulu usaili huo ni kama yalivyoorodheshwa katika tangazo hili.
Orodha ya majina haya pia inajumuisha baadhi ya wasailiwa waliokuwa kwenye kanzidata (Database) kwa kada mbalimbali ambao wamepangiwa vituo vya kazi baada ya nafasi kupatikana Wasailiwa wote waliofaulu usaili na kupangiwa vituo vya kazi, BARUA zao za kupangiwa vituo vya kazi watazipata kupitia AKAUNTI zao za Ajira Portal kwenye sehemu ya My Applications, hivyo watapaswa kupakua na kutoa nakala (Download and Print) barua hizo na Kwenda nazo kuripoti katika vituo vya kazi walivyopangiwa.
Aidha, waombaji kazi waliofaulu usaili na kupangiwa kituo cha kazi wanatakiwa kuripoti kwa Mwajiri katika muda ambao umeainishwa kwenye barua za kupangiwa kituo cha kazi wakiwa na vyeti halisi (Originals Certificates) za masomo kuanzia kidato cha nne na kuendelea ili vihakikiwe na mwajiri kabla ya kupewa barua ya Ajira. Kwa wale ambao majina yao hayapo katika tangazo hili watambue kuwa hawakupata nafasi/hawa kufaulu usaili, hivyo wasisite kuomba kwa mara nyingine nafasi za kazi zitakapo tangazwa.
View the full list here
11 days left to report
Share this opportunity
Help others find their dream job
