Tangazo la Kuitwa Kazini Taasisi Mbalimbali za Umma 23-12-2025

Job Role Insights

  • Date posted

    2025-12-24

  • Closing date

    2026-01-06

  • Hiring location

    Tanzania

  • Quantity

    10 person

  • Gender

    both

  • Job ID

    126434

Job Description

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma anatoa taarifa kwa waombaji kazi waliofanya usaili kati ya tarehe 23-04-2025 na tarehe 19-11-2025 kuhusu matokeo ya usaili na upangaji wa vituo vya kazi.

MATOKEO YA USAILI NA UPANGAJI WA VITUO

Matokeo ya waombaji kazi waliofaulu usaili huo ni kama yalivyoorodheshwa katika tangazo hili. Orodha hii pia inajumuisha baadhi ya wasailiwa waliokuwa kwenye kanzidata (Database) kwa kada mbalimbali ambao wamepangiwa vituo vya kazi baada ya nafasi kupatikana.

UTARATIBU WA KUPATA BARUA ZA KUPANGIWA KAZI

Wasailiwa wote waliofaulu na kupangiwa vituo vya kazi watazipata barua zao kupitia AKAUNTI zao za Ajira Portal.

  • Mtumiaji anapaswa kuingia kwenye akaunti yake na kwenda sehemu ya My Applications.
  • Ni lazima kupakua na kutoa nakala (Download and Print) ya barua hizo.
  • Barua hizo ndizo zitakazotumika kuripoti katika vituo vya kazi walivyopangiwa.

MAHITAJI NA MUDA WA KURIPOTI

Waombaji waliofaulu wanatakiwa kuripoti kwa Mwajiri katika muda ambao umeainishwa kwenye barua zao. Wakati wa kuripoti, mhusika anapaswa kuwa na:

  • Vyeti halisi (Original Certificates) za masomo kuanzia kidato cha nne na kuendelea.
  • Vyeti hivi vitahakikiwa na mwajiri kabla ya mhusika kupewa barua ya Ajira.

TAARIFA KWA WALE AMBAO HAWAJAFAULU

Kwa waombaji ambao majina yao hayapo katika tangazo hili, watambue kuwa hawakupata nafasi au hawakufaulu usaili kwa wakati huu. Sekretarieti inawahimiza wasisite kuomba kwa mara nyingine nafasi za kazi zitakapotangazwa hapo baadaye.

View the full list here

13 days left to report

View Names

Share this opportunity

Help others find their dream job

How to Apply

View Names
Send message
Cancel