Nafasi za Kazi 31 Chama cha Walimu Tanzania (CWT)

Job Role Insights

  • Date posted

    2026-08-20

  • Closing date

    2026-09-01

  • Hiring location

    Dodoma

  • Career level

    Middle

  • Qualification

    Certificate Degree Diploma High School Certificate O-Level Secondary Education Vocational / Technical

  • Experience

    1 - 2 Years

  • Quantity

    31 person

  • Gender

    both

  • Job ID

    142034

Job Description

The total number of job posts listed here for the Tanzania Teachers Union (Chama cha Walimu Tanzania - CWT) is 31 posts in August 2026.

This trade union recruitment targets legal representation and office management support across CWT's regional, district, and headquarters offices in Mainland Tanzania.

Job Title / SpecializationPosts
Katibu Muhtasi (Personal Secretary / Secretarial Assistant)27
Mwanasheria (Legal Officer / Advocate)4
TOTAL POSTS31

Chama cha Walimu Tanzania (CWT) ni chama cha wafanyakazi kutoka kada ya walimu ambacho shughuli zake zipo Tanzania Bara. Chama kimesajiliwa kwa Namba 004 chini ya Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini Na. 6 ya mwaka 2004 na kinaajiri wafanyakazi kwa ajira ya kudumu katika mikoa, wilaya na makao makuu.

Ili kuboresha huduma kwa wanachama, CWT kinatangaza nafasi za ajira kwa Katibu Muhtasi na Mwanasheria kwa Watanzania wenye sifa ambao watakuwa tayari kufanya kazi mahali popote Tanzania.

1. Katibu Muhtasi - Nafasi 27

Sifa za Mwombaji

  • Awe amehitimu Kidato cha Nne au zaidi.
  • Awe na Cheti cha NTA Level 4, 5 au 6 cha Uhazili kinachotambuliwa na NACTE.
  • Awe na uzoefu wa kutumia kompyuta na intaneti.
  • Awe na uwezo wa kutumia lugha ya Kiswahili na Kiingereza kwa ufasaha.
  • Awe na uzoefu wa kazi usiopungua miaka miwili.

Majukumu ya Kazi

  • Kupiga chapa nyaraka mbalimbali za Chama.
  • Kutunza kumbukumbu mbalimbali kama atakavyoelekezwa na mkuu wake wa kazi.
  • Kupokea wageni na kuwaelekeza mahali wanapoweza kusaidiwa.
  • Kupokea mawasiliano mbalimbali ya ofisi na kumpatia msimamizi wa kazi.
  • Kufanya usafi katika ofisi za Chama.
  • Kutunza siri zote za ofisi.
  • Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa na msimamizi wa kazi.

2. Mwanasheria - Nafasi 4

Sifa za Mwombaji

  • Awe na Shahada ya Kwanza ya Sheria (LLB) kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali.
  • Awe amehudhuria Shule ya Sheria (School of Law) na kuapishwa kama Wakili.
  • Awe na uwezo wa kuzungumza na kuandika kwa ufasaha kwa lugha ya Kiswahili na Kiingereza.
  • Awe na uwezo wa kutumia kompyuta.
  • Awe raia wa Tanzania.
  • Mwombaji mwenye taaluma ya Ualimu atapewa kipaumbele.

Majukumu ya Kazi

  • Kusimamia kesi mbalimbali za Chama na wanachama katika Mahakama na taasisi zenye mamlaka ya kusikiliza mashauri.
  • Kusoma na kutafsiri sheria na maandiko mbalimbali ya kisheria.
  • Kutoa ushauri wa kisheria kwa walimu na Chama.
  • Kutatua migogoro ya kikazi wanayokabiliana nayo walimu.
  • Kufuatilia utekelezaji wa changamoto mbalimbali za walimu katika ofisi za Serikali na kwa waajiri.

Masharti ya Jumla

  • Waombaji wote wawe raia wa Tanzania.
  • Waombaji wawe na umri usiozidi miaka 45.
  • Waombaji waambatishe cheti cha kuzaliwa.
  • Waombaji waambatishe maelezo binafsi yanayojitosheleza (Detailed CV) yenye anwani na namba za simu za kuaminika.
  • CV iwe na majina na mawasiliano ya wadhamini (referees) watatu wa kuaminika.
  • Maombi yaambatane na vyeti vya taaluma na nakala za vyeti husika.
  • Waombaji waambatishe cheti cha mtihani wa Kidato cha IV na Kidato cha VI kwa wale waliofikia kiwango hicho.
  • Waombaji waambatishe vyeti vya kitaaluma na vyeti vya mafunzo mbalimbali vinavyohusiana na sifa za kazi husika.
  • Waombaji wawe na uzoefu wa kazi usiopungua miaka miwili.
  • Waombaji wawe na uwezo wa kutumia lugha ya Kiswahili na Kiingereza kwa ufasaha.
  • Waombaji wawasilishe picha moja ya passport size ya hivi karibuni na kuandika jina nyuma ya picha.
  • Waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe vyeti vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa na mamlaka husika, ikiwemo TCU na NECTA.
  • Uwasilishaji wa taarifa au sifa za kughushi utasababisha wahusika kuchukuliwa hatua za kisheria.
  • Maombi yanaweza kuandikwa kwa lugha ya Kiswahili au Kiingereza.
  • Waombaji watakaokidhi vigezo pekee ndio watakaoitwa kwenye usaili.

Jinsi ya Kutuma Maombi

Maombi yote yawasilishwe kwa:

Katibu Mkuu
Chama cha Walimu Tanzania (CWT)
S.L.P. 3077
Dodoma, Tanzania

Barua pepe: [email protected]

Mwisho wa Kutuma Maombi: 01 Septemba 2026, saa 10:00 jioni.

Mwajiri: Chama cha Walimu Tanzania (CWT)

Mahali pa Kazi: Tanzania Bara, kulingana na mahitaji ya Chama.

Interested in this job?

12 days left to apply

Apply now

Your job search, in your pocket

Get the ZoomTanzania Jobs app - apply on the go, get instant job alerts, and chat with our AI assistant anytime, anywhere.

How to Apply

Maombi yote yawasilishwe kwa: Katibu Mkuu Chama cha Walimu Tanzania (CWT) S.L.P. 3077 Dodoma, Tanzania Barua pepe: [email protected] Mwisho wa Kutuma Maombi: 01 Septemba 2026, saa 10:00 jioni.

Apply now