Meneja (Nafasi 1) Bodi ya DUWASA Saccos Ltd

by DUWASA Saccos Ltd in
47 (views)

Job Role Insights

  • Date posted

    2026-05-05

  • Closing date

    2026-05-18

  • Hiring location

    Dodoma

  • Career level

    Middle

  • Qualification

    Bachelor Degree

  • Experience

    3 - 5 Years

  • Quantity

    1 person

  • Gender

    both

  • Job ID

    131530

Job Description

TANGAZO LA NAFASI YA KAZI

CHAMA CHA AKIBA NA MIKOPО DUWASA SACCOS LTD

KUHUSU DUWASA SACCOS DUWASA Savings and Credit Co-operative Society (DUWASA Saccos) ni ushirika wa akiba na mikopo uliopo jijini Dodoma kilichoanzishwa chini ya Sheria ya Vyama vya Ushirika Na.20 ya Mwaka 2003 na kurekebishwa mwaka 2013. Saccos hii imeundwa na wafanyakazi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA) kwa lengo la kuinua hali ya kiuchumi ya wanachama wake kupitia huduma bora za kifedha, mikopo nafuu, na elimu ya uwekezaji.

Meneja (Nafasi 1)

Bodi ya DUWASA Saccos Ltd inakusudia kuajiri Meneja mwenye uwezo, ujuzi na uzoefu wa kutosha katika Kusimamia na kuendesha shughuli zinazohusu Ushirika wa Akiba na Mikopo. Meneja / Katibu wa Chama atakuwa ndiye Msimamizi wa shughuli zote za Chama za kila siku kulingana na Miongozo iliyopo na maelekezo yatakayotolewa na Bodi.

ELIMU NA UJUZI:

  • I. Awe na shahada ya uhasibu au shahada ya uongozi, uchumi au biashara katika chuo kinachotambulika na kusajiliwa na serikali.
  • II. Awe na uzoefu wa kazi usiopungua miaka mitatu (3).
  • III. Awe na uwezo wa kuandika na kuongea Kiswahili na Kiingereza kwa ufasaha.
  • IV. Awe na uwezo wa kujituma na kufanya kazi bila kutegemea mtu mwingine.
  • V. Awe mbunifu katika uendelezaji wa shughuli za chama.
  • VI. Awe na uwezo wa kuandaa hesabu za chama na kuziwasilisha kwenye bodi ya chama, wanachama na wadau wengine.

MAJUKUMU YA NAFASI YA MENEJA

  • I. Kusimamia shughuli zote za kiutendaji na kifedha za Saccos.
  • II. Kuandaa na kutekeleza mpango mkakati na bajeti ya mwaka.
  • III. Kuhakikisha utunzaji sahihi wa kumbukumbu za fedha na wanachama.
  • IV. Kuandaa taarifa za fedha za kila mwezi na mwaka.
  • V. Kusimamia ukusanyaji wa madeni na kuzuia limbikizo la mikopo.
  • VI. Kuwa kiungo kati ya Bodi ya Wakurugenzi, wanachama, na mamlaka za udhibiti.

MAMBO YA KUZINGATIA KWA MWOMBAJI:

  • I. Muombaji wa kazi lazima awe ni Raia wa Tanzania mwenye umri usiopungua miaka 18 na usiozidi miaka 45.
  • II. Muombaji kazi sharti aambatishe cheti cha kuzaliwa.
  • III. Muombaji kazi aambatishe maelezo binafsi yanayojitosheleza (Detailed C.V) yenye anwani na namba za simu zinazopatikana pamoja na majina ya Wadhamini (referees) watatu wa kuaminika.
  • IV. Maombi yote yaambatane na nakala za vyeti vya taaluma, nakala ya vyeti vya kidato cha nne au kidato cha sita kwa wale waliofikia kiwango hicho na vyeti vya kuhitimu mafunzo ngazi mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi hii.
  • V. "Testimonials", "Provisional Results", "Statement of results", hati matokeo za kidato cha nne na sita (FORM IV AND FORM VI RESULTS SLIPS) HAVITAKUBALIWA.
  • VI. Maombi yatakayowasilishwa nje ya utaratibu ulioainishwa katika tangazo hili HAYATAFIKIRIWA.
  • VII. Kumbuka kuambatisha barua yako ya maombi ya kazi iliyosainiwa na kuandikwa kwa lugha ya Kiswahili au Kiingereza na barua hiyo ielekezwe kwa anwani hapo chini na mwisho wa kutuma maombi ya kazi ni siku ya Jumapili, tarehe 31/05/2026 saa 5:59 usiku.
  • VIII. Waombaji wenye sifa wanatakiwa kutuma barua za maombi, wasifu (CV), na nakala za vyeti vya taaluma kwa:

MWENYEKITI WA BODI CHAMA CHA AKIBA NA MIKOPО, DUWASA BARABARA YA MKAPA, SLP 431 DODOMA Barua pepe: [email protected]

Imetolewa leo tarehe 03/05/2026 DUWASA SACCOS LTD

Interested in this job?

13 days left to apply

Apply now

Share this opportunity

Help others find their dream job

Generate Cover Letter

Login as a candidate to generate a free AI cover letter for this job

How to Apply

MWENYEKITI WA BODI CHAMA CHA AKIBA NA MIKOPО, DUWASA BARABARA YA MKAPA, SLP 431 DODOMA Barua pepe: [email protected] Imetolewa leo tarehe 03/05/2026 DUWASA SACCOS LTD

Apply now
Send message
Cancel